1Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
2wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana):
Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
3wazao wa Paroshi2,172
4wazao wa Shefatia372
5wazao wa Ara775
6wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu)2,812
7wazao wa Elamu1,254
8wazao wa Zatu945
9wazao wa Zakai760
10wazao wa Bani642
11wazao wa Bebai623
12wazao wa Azgadi1,222
13wazao wa Adonikamu666
14wazao wa Bigwai2,056
15wazao wa Adini454
16wazao wa Ateri (kupitia Hezekia)98
17wazao wa Besai323
18wazao wa Yora112
19wazao wa Hashumu223
20wazao wa Gibari95
21watu wa Bethlehemu123
22watu wa Netofa56
23watu wa Anathothi128
24watu wa Azmawethi42
25wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi743
26wazao wa Rama na Geba621
27watu wa Mikmashi122
28watu wa Betheli na Ai223
29wazao wa Nebo52
30wazao wa Magbishi156
31wazao wa Elamu ile ingine1,254
32wazao wa Harimu320
33wazao wa Lodi, Hadidi na Ono725
34wazao wa Yeriko345
35wazao wa Senaa3,630
36Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua)973
37wazao wa Imeri1,052
38wazao wa Pashuri1,247
39wazao wa Harimu1,017
40Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia)74
41Waimbaji: wazao wa Asafu128
42Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao waShalumu, Ateri, Talmoni,Akubu, Hatita na Shobai139
43Watumishi wa Hekalu:*wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
44wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
45wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
46wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
47wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
48wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
49wazao wa Uza, Pasea, Besai,
50wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
51wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
52wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
53wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
54wazao wa Nesia na Hatifa.
55Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
56wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
57wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
58Watumishi wa Hekalu wote nawazao wa watumishiwa Solomoni392
59Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
60wazao waDelaya, Tobia na Nekoda652
61Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
62Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
63Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.*
64Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
65tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
66Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
67ngamia 435 na punda 6,720.
68Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
69Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000*za dhahabu, mane 5,000*za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
70Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.
Tanbihi
Yaani Wanethini (pia 2:58, 70).
Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha kifuani cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha.
Darkoni 61,000 za dhahabu ni sawa na kilo 500.
Mane 5,000 za fedha ni sawa na kilo 2,900.