Inapakia...
📖

Biblia Takatifu

Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™
BIB 24 mistari

Yoshua 12

Yoshua • Sura 12 / 24

Orodha Ya Wafalme Walioshindwa

1Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:

2Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.

3Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi*hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi*), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.

4Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.

5Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.

6Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.

7Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:

8nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):

9mfalme wa Yerikommojamfalme wa Ai (karibu na Betheli)mmoja

10mfalme wa Yerusalemummojamfalme wa Hebronimmoja

11mfalme wa Yarmuthimmojamfalme wa Lakishimmoja

12mfalme wa Eglonimmojamfalme wa Gezerimmoja

13mfalme wa Debirimmojamfalme wa Gederimmoja

14mfalme wa Hormammojamfalme wa Aradimmoja

15mfalme wa Libnammojamfalme wa Adulamummoja

16mfalme wa Makedammojamfalme wa Bethelimmoja

17mfalme wa Tapuammojamfalme wa Heferimmoja

18mfalme wa Afekimmojamfalme wa Lasharonimmoja

19mfalme wa Madonimmojamfalme wa Hazorimmoja

20mfalme wa Shimron-Meronimmojamfalme wa Akishafummoja

21mfalme wa Taanakimmojamfalme wa Megidommoja

22mfalme wa Kedeshimmojamfalme wa Yokneamu katika Karmelimmoja

23mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori)*mmojamfalme wa Goimu katika Gilgalimmoja

24mfalme wa Tirsammoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

Tanbihi

*

Yaani Bahari ya Galilaya.

*

Yaani Bahari Mfu.

*

Au: katika miinuko ya Nafoth-Dori.