1Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3Nikawaambia, āMalango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.ā
4Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana):
Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8wazao wa Paroshi2,172
9wazao wa Shefatia372
10wazao wa Ara652
11wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu)2,818
12wazao wa Elamu1,254
13wazao wa Zatu845
14wazao wa Zakai760
15wazao wa Binui648
16wazao wa Bebai628
17wazao wa Azgadi2,322
18wazao wa Adonikamu667
19wazao wa Bigwai2,067
20wazao wa Adini655
21wazao wa Ateri (kupitia Hezekia)98
22wazao wa Hashumu328
23wazao wa Besai324
24wazao wa Harifu112
25wazao wa Gibeoni95
26watu wa Bethlehemu na Netofa188
27watu wa Anathothi128
28watu wa Beth-Azmawethi42
29watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi743
30watu wa Rama na Geba621
31watu wa Mikmashi122
32watu wa Betheli na Ai123
33watu wa Nebo52
34wazao wa Elamu1,254
35wazao wa Harimu320
36wazao wa Yeriko345
37wazao wa Lodi, Hadidi na Ono721
38wazao wa Senaa3,930
39Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua)973
40wazao wa Imeri1,052
41wazao wa Pashuri1,247
42wazao wa Harimu1,017
43Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia)74
44Waimbaji: wazao wa Asafu148
45Mabawabu wa malango: wazao waShalumu, Ateri, Talmoni,Akubu, Hatita na Shobai138
46Watumishi wa Hekalu:*wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56wazao wa Nesia na Hatifa.
57Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni392
61Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
62wazao waDelaya, Tobia na Nekoda642
63Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65Kwa hiyo, mtawala*aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.*
66Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
68Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69ngamia 435 na punda 6,720.
70Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000*za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu,*na mane 2,200*za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ezra Asoma Sheria Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,
Tanbihi
Yaani Wanethini(pia 7:60, 73).
Au Tirshatha: jina la heshima aliloitwa mtawala wa Yuda chini ya Ufalme wa Uajemi (pia 7:70).
Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha juu cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha.
Darkoni 1,000 za dhahabu ni sawa na uzito wa kilo 8.6.
Darkoni 20,000 za dhahabu ni sawa na kilo 172.
Mane 2,200 za fedha ni sawa na kilo 1,300.