Inapakia...
📖

Biblia Takatifu

Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™
BIB 8 mistari

Zaburi 101

Zaburi • Sura 101 / 150

Ahadi Ya Kuishi Kwa Uadilifu Na Kwa Haki
Zaburi ya Daudi.

1Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako;kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.

2Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama:utakuja kwangu lini?
Nitatembea nyumbani mwangukwa moyo usio na lawama.

3Sitaweka mbele ya macho yangukitu kiovu.
Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani;hawatashikamana nami.

4Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami;nitajitenga na kila ubaya.

5Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri,huyo nitamnyamazisha;mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburihuyo sitamvumilia.

6Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,ili waweze kuishi pamoja nami;yeye ambaye moyo wake hauna lawamaatanitumikia.

7Mdanganyifu hatakaanyumbani mwangu,yeye asemaye kwa uongohatasimama mbele yangu.

8Kila asubuhi nitawanyamazishawaovu wote katika nchi;nitamkatilia mbali kila mtenda mabayakutoka mji wa Bwana.