1Kama vile ayala aoneavyo shauku vijito vya maji,ndivyo nafsi yangu ikuoneavyo shauku, Ee Mungu.
2Nafsi yangu inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye hai.Ni lini nitaweza kwenda kukutana na Mungu?
3Machozi yangu yamekuwa chakula changuusiku na mchana,huku watu wakiniambia mchana kutwa,“Yuko wapi Mungu wako?”
4Mambo haya nayakumbukaninapoimimina nafsi yangu:Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu,nikiongoza maandamano kuelekea kwenye nyumba ya Mungu,kwa kelele za shangwe na za shukranikatikati ya umati uliosherehekea.
5Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?Weka tumaini lako kwa Mungu,kwa sababu bado nitamsifu,
Mwokozi wangu na
6
Mungu wangu.
Nafsi yangu inasononeka ndani yangu;kwa hiyo nitakukumbukakutoka nchi ya Yordani,katika vilele vya Hermoni,
kutoka Mlima Mizari.
7Kilindi huita kilindi,katika ngurumo za maporomoko ya maji yako;mawimbi yako yote pamoja na viwimbivimepita juu yangu.
8Mchana Bwana huelekeza upendo wake,usiku wimbo wake uko nami:
maombi kwa Mungu wa uzima wangu.
9Ninamwambia Mungu Mwamba wangu,“Kwa nini umenisahau?Kwa nini niendelee kuomboleza,nikiwa nimeonewa na adui?”
10Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makaliadui zangu wanaponidhihaki,wakiniambia mchana kutwa,“Yuko wapi Mungu wako?”
11Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?Weka tumaini lako kwa Mungu,kwa sababu bado nitamsifu,
Mwokozi wangu na Mungu wangu.