1Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2Bwana anayapenda malango ya Sayuni
kuliko makao yote ya Yakobo.
3Mambo matukufu yanasemwa juu yako,ee mji wa Mungu:
4“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu*na Babelimiongoni mwa wale wanaonikubali mimi:Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,*nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”
5Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,“Huyu na yule walizaliwa humo,naye Aliye Juu Sana mwenyeweatamwimarisha.”
6Bwana ataandika katika orodha ya mataifa:“Huyu alizaliwa Sayuni.”
7Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
Tanbihi
Rahabu hapa ni jina la ushairi la Misri.
Kushi hapa ina maana ya Naili ya juu, yaani Ethiopia.