1Katika siku ile utasema:“Nitakusifu wewe, Ee Bwana.Ingawa ulinikasirikia,hasira yako imegeukia mbalinawe umenifariji.
2Hakika Mungu ni wokovu wangu;nitamtumaini wala sitaogopa.Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu;amekuwa wokovu wangu.”
3Kwa furaha mtachota majikutoka visima vya wokovu.
4Katika siku hiyo mtasema:“Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake;julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu,hili na lijulikane duniani kote.
6Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”