Inapakia...
📖

Biblia Takatifu

Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™
BIB 17 mistari

Isaya 54

Isaya • Sura 54 / 66

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

1“Imba, ewe mwanamke tasa,wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,wewe ambaye kamwe hukupata utungu;kwa sababu watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengikuliko wa mwanamke mwenye mume,”asema Bwana.

2“Panua mahali pa hema lako,tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,
wala usiyazuie;ongeza urefu wa kamba zako,imarisha vigingi vyako.

3Kwa maana utaenea upande wa kuumena upande wa kushoto;wazao wako watayamiliki mataifana kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

4“Usiogope, wewe hutaaibika.Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.Wewe utasahau aibu ya ujana wako,wala hutakumbuka tena mashutumu ya ujane wako.

5Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

6Bwana atakuita urudikana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni;kama mke aliyeolewa bado angali kijanana kukataliwa,” asema Mungu wako.

7“Kwa kitambo kidogo nilikuacha,lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

8Katika ukali wa hasiranilikuficha uso wangu kwa kitambo,lakini kwa fadhili za milelenitakuwa na huruma juu yako,”
asema Bwana Mkombozi wako.

9“Kwangu mimi jambo hili ni kama siku za Noa,nilipoapa kuwa maji ya Noa kamwe hayatafunika tena dunia.Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,kamwe sitawakemea tena.

10Ijapotikisika milima, na vilima viondolewe,hata hivyo upendo wangu usiokoma kwenu hautatikisika,wala agano langu la amani halitaondolewa,”asema Bwana, mwenye huruma juu yenu.

11“Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba na usiyetulizwa,nitakujenga kwa almasi, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

12Nitafanya minara yako ya akiki,malango yako kwa vito vingʼaavyo,
nazo kuta zako zote za vito vya thamani.

13Watoto wako wote watafundishwa na Bwana,nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

14Kwa haki utathibitika:
Kuonewa kutakuwa mbali nawe;hutaogopa chochote.Hofu itakuwa mbali nawe;haitakukaribia wewe.

15Kama mtu yeyote akikushambulia,haitakuwa kwa ruhusa yangu;yeyote akushambuliayeatajisalimisha kwako.

16“Tazama, ni mimi niliyemuumba mhunzi,yeye afukutaye makaa kuwa moto,
na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.Tena ni mimi niliyemwambia mharabukufanya uharibifu mwingi.

17Hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yakoitakayofanikiwa,nawe utauthibitisha kuwa mwongokila ulimi utakaokushtaki.Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwanana hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”asema Bwana.