Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1Moyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,macho yangu hayajivuni;sijishughulishi na mambo makuu kunizidiwala mambo ya ajabu mno kwangu.
2Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,kama mtoto aliyeachishwa kunyonyandivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.
3Ee Israeli, mtumaini Bwanatangu sasa na hata milele.