Mungu Mfalme
1Bwana anatawala, amejivika utukufu;Bwana amejivika utukufu
tena amejivika nguvu.Dunia imewekwa imara,haitaondoshwa.
2Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;wewe umekuwako tangu milele.
3Bahari zimeinua, Ee Bwana,bahari zimeinua sauti zake;
bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.
4Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:
Bwana aishiye juu sana ni mkuu.
5Ee Bwana, sheria zako ni imara;utakatifu umepamba nyumba yako
pasipo mwisho.