1Mimi ni ua la Sharoni,yungiyungi ya bondeni.
2Kama yungiyungi katikati ya miibandivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali.
3Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msitunindivyo alivyo mpenzi wangu
miongoni mwa wanaume vijana.Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu,na tunda lake ni tamu kwangu.
4Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu,na bendera ya huyu mwanaume
juu yangu ni upendo.
5Nitie nguvu kwa zabibu kavu,niburudishe kwa matofaa,
kwa maana ninazimia kwa mapenzi.
6Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,na mkono wake wa kuume unanikumbatia.
7Binti za Yerusalemu, ninawaagizakwa paa na kwa ayala wa shambani:Msichochee wala kuamsha mapenzihata yatakapotaka yenyewe.
8Sikiliza! Mpenzi wangu!Tazama! Huyu hapa anakuja,akirukaruka juu milimaniakizunguka juu ya vilima.
9Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana.Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu,akitazama kupitia madirishani,akichungulia kimiani.
10Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia,“Inuka, mpenzi wangu,
mrembo wangu, tufuatane.
11Tazama! Wakati wa masika umepita,mvua imekwisha na ikapita.
12Maua yanatokea juu ya nchi;majira ya kuimba yamewadia,sauti za njiwa zinasikikakatika nchi yetu.
13Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni,zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri.Inuka, njoo mpenzi wangu.Mrembo wangu, tufuatane.”
14Hua wangu penye nyufa za majabali,mafichoni pembezoni mwa mlima,nionyeshe uso wako,na niisikie sauti yako,kwa maana sauti yako ni tamu,na uso wako unapendeza.
15Tukamatie mbweha,mbweha wale wadogowanaoharibu mashamba ya mizabibu,mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua.
16Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake,yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
17Mpaka jua linapochomoza,na vivuli vikimbie,rudi, mpenzi wangu,na uwe kama paa,au kama ayala kijanajuu ya vilima vya Betheri.