1Wamenionea mno tangu ujana wangu;Israeli na aseme sasa:
2wamenionea mno tangu ujana wangu,lakini bado hawajanishinda.
3Wakulima wamelima mgongo wangu,na kufanya mifereji yao mirefu.
4Lakini Bwana ni mwenye haki;amenifungua toka kamba za waovu.
5Wale wote waichukiao Sayunina warudishwe nyuma kwa aibu.
6Wawe kama majani juu ya paa,ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8Wale wapitao karibu na wasiseme,“Baraka ya Bwana iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Bwana.”