Inapakia...
📖

Biblia Takatifu

Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™
BIB 11 mistari

Zaburi 29

Zaburi • Sura 29 / 150

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba
Zaburi ya Daudi.

1Mpeni Bwana, enyi mashujaa,mpeni Bwana utukufu na nguvu.

2Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3Sauti ya Bwana iko juu ya maji;Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.

4Sauti ya Bwana ina nguvu;sauti ya Bwana ni tukufu.

5Sauti ya Bwana huvunja mierezi;Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.

6Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,Sirioni*urukaruke kama mwana nyati.

7Sauti ya Bwana hupiga kwa mialiya umeme wa radi.

8Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.

9Sauti ya Bwana huzalisha ayala,na huuacha msitu wazi.Hekaluni mwake wote wasema,“Utukufu!”

10Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.

11Bwana huwapa watu wake nguvu;Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

Tanbihi

*

Yaani Mlima Hermoni.